• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

MAAFISA WAANDISHI WASAIDIZI WAPATA MAFUNZO YA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Posted on: August 30th, 2024


Akianza kwa kuwapongeza Maafisa Waandishi Wasaidizi Ngazi ya Kata  kwa kupata nafasi ya kuteuliwa na kuendesha zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Afisa Mwandikishaji Jimbo la Bariadi Ndg. Halidi M. Mbwana alisema hana shaka na uteuzi wao kwakuwa umetokana na ujuzi,uwezo na weledi walio nao katika kutekeleza majukumu ya kitaifa ikiwemo Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.


Hayo aliyasema Jana wakati akifungua rasmi mafunzo kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Maafisa Waandishi Wasaidizi Ngazi ya Kata yaliyofanywa Makao Makuu ya  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.


" Hiki tunachokifanya ni maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025,wapiga kura hawa ambao tutawaandikisha leo, ndio wapiga kura ambao watashiriki kwenye zoezi la Uchaguzi wa mwaka 2025. Kwahiyo ninyi mmeaminiwa na hatuna shaka juu ya hilo.Nimatumaini yangu kutokana na semina hii kila mtu atapata elimu ya kutosha itakayomwezesha kufanya majukumu yake ili kufanikisha zoezi hili. Mafunzo haya yatausisha namna bora ya ujazaji wa fomu, kutumia mfumo wa waandikishaji wapiga kura (Voters registration system,VRS), pamoja na matumizi sahihi ya vifaa uandikishaji wapiga kura." Alisema Afisa Mwandikishaji huyo.


Aidha alisisitiza kuwa baada ya mafunzo hayo wataenda kutoa mafunzo kwa waandishi Wasaidizi na waendeshaji vifaa vya Bayometriki tarehe 1-2/09/2024.Amesema wanapaswa kuwa makini na kuelewa kama jinsi yeye na timu yawafundishaji walivyofundishwa wakaelewa na kuwafundisha wao, na wao watapaswa kwenda kuwafundisha wengine ili kufanikisha zoezi.


Amekumbusha katika maeneo ambayo zoezi la uandikishaji litafanyika, Mawakala wa kisiasa waeneo husika wameruhusiwa kuwepo ili kuleta uwazi katika zoezi zima na kutambua wapiga kura wa eneo husika na hata kupunguza vurugu zisizo za lazima.Amekazia kuwa Mawakala hao hawatakiwi kuingilia utekelezaji wa majukumu yao wakati wa zoezi la uandikishaji likifanyika.


Kutokana na matokeo ya mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi Tanzania ( Sensa 2022), Mkoa wa Simiyu una idadi ya watu 2,140,497,ikiwa wenye umri kati ya miaka 15-64 ni  45.6% na miaka 60 kuendeleza ni 4.7% ambao kwa asilimia kubwa wako kwenye kundi la wapigaji kura.

#bariadidc

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.