• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

MAENDELEO YA MRADI WA UTUNZAJI WA MAZINGIRA – SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MKOA WA SIMIYU

Posted on: September 10th, 2025



Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkoa wa Simiyu imefanikiwa kutekeleza mradi mkubwa wa utunzaji wa mazingira wenye thamani ya Tsh. milioni 2.13. Mradi huu umefadhiliwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa mazingira wakiwemo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Alliance Ginnery Co. Ltd na Shirika la Trees for the Future.

 Mradi huu umejikita katika Kijiji cha Igegu, Kata ya Sapiwi na ulikaguliwa rasmi na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 chini ya Kiongozi wa Mbio, Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava, tarehe 05/08/2024.

Lengo kuu la mradi ni kutekeleza sera ya Taifa ya upandaji miti, inayotaka kila Halmashauri kupanda angalau miti milioni 1.5 kwa mwaka. Katika hatua hii, shule imepanda:

  • Miti ya vivuli 805
  • Miti ya matunda 211

Kupitia miti hii, mradi unasaidia:
-Kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi
- Kulinda majengo ya shule dhidi ya upepo mkali
- Kuwapatia wanafunzi kivuli na matunda kwa afya bora
- Kuboresha mandhari ya shule na kupunguza vumbi

Hadi sasa, miti yote 1,016 imeota na inakua vizuri. Shule imepata mandhari ya kijani na hali ya hewa imeanza kuboreka. Aidha, inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2027, zaidi ya miti 500 ya matunda itaanza kutoa mazao, jambo litakaloongeza lishe ya wanafunzi na kuchangia usalama wa chakula kwa jamii inayoizunguka shule.

Ili kuhakikisha miti inatunzwa na kukua vizuri, zimeanzishwa hatua thabiti za ufuatiliaji na matunzo:

  • Kamati ya Mazingira ya shule na Serikali ya Kijiji zimepewa jukumu la uangalizi.
  • Klabu ya Mazingira ya wanafunzi na walimu inahamasishwa kushiriki moja kwa moja kwenye kumwagilia na kutunza miti.
  • Halmashauri na wadau wanaendelea kutoa elimu ya mazingira pamoja na vifaa vya kusaidia matunzo.

Mradi huu ni mfano wa mshikamano wa kijamii na jitihada za pamoja katika kulinda mazingira, kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wasichana wa Mkoa wa Simiyu.

 Kupitia hatua hizi, Simiyu Girls inabaki kuwa shule kinara katika kuhamasisha vizazi vipya kuhusu utunzaji wa mazingira na maendeleo endelevu.

#ClimateChange

#SimiyuMazingira

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MAENDELEO YA MRADI WA UTUNZAJI WA MAZINGIRA – SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MKOA WA SIMIYU

    September 10, 2025
  • MAENDELEO YA MRADI WA UJENZI WA BWENI NA UZIO – SHULE YA MSINGI IGAGANULWA

    September 03, 2025
  • Vijana Wachapakazi Banemhi Wafanikiwa Kupitia Mradi wa Bodaboda

    September 01, 2025
  • Nigo Lodge – Nguzo ya Maendeleo Igaganulwa, Bariadi

    August 26, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.