• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

MAPAMBANO YA KUDHIBITI UKIMWI YAENDELEA KWA KASI MPYA WILAYA YA BARIADI.

Posted on: October 6th, 2023

Katika kikao cha Kamati ya Kudhibiti UKIMWI kilichofanyika halmashauri ya Wilaya ya Bariadi leo,  kamati imeweza kubainisha matokeo ya shughuli  ziliyofanywa na halmashauri ambazo zimeleta taswira mpya katika mapambano dhidi kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa mwaka 2023/2024 katika wilaya yote.


Kamati hiyo  ikishirikiana na idara ya afya pamoja na wadau mbalimbali katika mapambano  dhidi ya VVU/UKIMWI kwa kipindi cha Julai -Septemba 2023 imeweza kutekeleza shughuli kubwa nne zilizoweza kusaidia kupunguwa kwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI. Shughuli hizo ni pamoja na kutoa huduma ya upimaji hiari wa VVU, ushauri nasaha, ushawishi wa mtoa huduma kupima na unasihi kwa mteja (HTC-CITC/PITC),kutoa huduma za tiba na matunzo, kutoa huduma ya kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) na huduma ya tohara kwa wanaume.


Kamati hiyo imewasilisha kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba 2023 jumla ya watu wapatao 4,879 wanaume wakiwa 2,098 sawa na 43% na wanawake 2,781 sawa na 57% walipima VVU na kati yao 79 walikutwa na maambukizi, kati yao   wanaume ni  25 sawa na 43.9% na wanawake ni 32 sawa na 56.1% ambayo kwa ujumla ni 1.6%.


Aidha katika kliniki ya baba, mama, na mtoto wateja waliopatikana  katika kupimwa wakati wa kliniki kabla ya kujifungua ni 5,205 kati yao  wateja  13 sawa na 0.25% waligundulika kuwa na maambukizi ya VVU. Wateja 1264 walipimwa wakati wa kujifungua na hakuna kati yao aliyebainika kuwa na maambukizi ya VVU. Mpango huu umesaidia sana kupunguza maambukizi dhidi ya virusi vya ukimwi.


Kamati hiyo imebainisha kuwa wateja wote waliobainika kuwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI waliweza kuanzishiwa kutumia dawa za kufubaza virusi kwa asilimia 100%. Aidha wateja 73 sawa 92.4% walianzishiwa kinga tiba ya kuwalinda wasipate maambukizi ya kifua kikuu.


Pia kamati imeidhininisha kuwa idara ya afya imeendelea kutekeleza afua ya Tohara Kinga kwa wanaume ili kuzuia maambukizi ikiwa kama njia mojawapo ambayo inasaidia kuzuia maambukizi ya UKIMWI kwa  asilimia 60%. Kwa kipindi cha Julai-Septemba 2023 idara imewafikia wanaume 597 sawa  na 79.2%  na lengo lilikuwa wanaume 754. Huduma hii ya tohara inatolewa kwa njia mbalimbali ikiwemo  huduma za ndani ya kituo cha afya na pia kupitia Huduma Mkoba ili kuwafikia wanaume wengi zaidi.


Akikazia katika kamati hiyo Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya Jamii, Bi. Beatrice Charles Gwamagobe amesema pamoja na kukazia sana katika usambazaji wa kondumu kwa ajili ya kujikinga na maambukizi pia halmashauri inapaswa kutoa elimu zaidi kuhusu UKIMWI na jinsi ya kupata lishe bora hasa kwa waathirika.


Akiongezea Mratibu wa UKIMWI na magonjwa ya ngono Dr. John Edward Mwaipungu amesema malengo ya dunia na Wizara ya Afya kwa ujumla ni, kufikia mwaka 2030 kuwe hakuna maambukizi mapya na pia wote ambao wameambukizwa  wawe kwenye matibabu  hususa ili watakapopima virusi vya maambukizi ya UKIMWI visiweze kuonekana  kwenye vipimo ikiwa ni moja ya matokeo mazuri ya matumizi ya  tiba  na lengo ni kufanikiwa  kuwa na  jamii huru bila maambukizi.


Katika kipindi cha Julai-Septemba 2023, halmashauri imeweza kusambaza katika jamii hasa katika nyumba za kulala wageni na maeneo ya uchimbaji madini kondomu za kiume 56,000 na kuwa inategemea kusambaza kondomu za kiume 800,000 sawa na 72%  kati ya kondomu 1,100,000 ambazo zitatumika kwa kipindi cha miezi mitatu, Octoba-Disemba 2023.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • DC BARIADI ONGOZA MDAHALO IKIWA NI MAADHIMISHO YA SIKU YA MUUNGANO

    April 26, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.