• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

NMB Yatangaza Gawio la TSh Milioni 750 Kurejesha kwa Jamii, Yaahidi Kuendelea Kusaidia Elimu na Afya Bariadi DC

Posted on: February 3rd, 2026

Bariadi, Februari 3, 2026


Meneja wa Benki ya NMB Tanzania, Tawi la Bariadi Mjini, Ndg. Andrew Msonga, leo Februari 3, 2026, ameongoza timu ya wataalamu wa Mikopo na Mahusiano ya benki hiyo kufanya ziara na mazungumzo na Menejimenti ya Kamati ya Ushauri ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.


Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika ndani ya ukumbi mdogo wa Halmashauri, Ndg. Msonga ametoa shukrani za dhati kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kwa ushirikiano mzuri walioutoa kwa Benki ya NMB katika mwaka 2025, hususan katika kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia watumishi na wadau mbalimbali kwa ufanisi.


Amesema pamoja na kuwasilisha salamu za heri ya mwaka mpya, lengo kuu la ziara hiyo ni kuujulisha uongozi wa Halmashauri kuwa Benki ya NMB Tanzania imeamua kurejesha gawio la TSh milioni 750 kwa jamii na wadau wake kama ishara ya shukrani kwa ushirikiano na mchango wao katika ukuaji wa benki na maendeleo ya taifa kwa ujumla.


Kwa mujibu wa Ndg. Msonga, gawio hilo litalenga kusaidia sekta muhimu za kijamii ikiwemo elimu, ambapo shule zitanufaika kwa kupatiwa madawati; sekta ya afya kwa kupatiwa vifaa tiba, hususan vinavyohusiana na huduma za uzazi; pamoja na utekelezaji wa programu maalum ya ufadhili wa elimu iitwayo “ *Nuru Yangu”* , inayosaidia wanafunzi kuanzia ngazi ya sekondari hadi elimu ya juu.


Ameeleza kuwa kupitia programu ya Nuru Yangu, jumla ya wahitimu wa vyuo 21 waliweza kuajiriwa mwaka huu, hatua inayoonesha mchango wa NMB katika kuendeleza rasilimali watu na kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana. Aidha, sehemu ya gawio hilo itatumika kukamilisha miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa masoko na stendi, kusaidia waathirika wa majanga ya asili, pamoja na kutoa msaada katika nyakati za mitihani na mahitaji mengine ya kijamii.


Katika kikao hicho, Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg. Steven Masunga, aliuliza kuhusu namna ambavyo NMB itaweza kusaidia changamoto ya upungufu wa madawati unaojitokeza kwa wanafunzi wanaoanza darasa la kwanza na kidato cha kwanza katika shule nyingi wilayani humo. Pia alieleza kuhusu mwanafunzi mmoja aliyefanya vizuri katika Mtihani wa Darasa la Saba na kuchaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Wavulana Kibaha, lakini anatoka katika familia isiyo na uwezo, hali iliyosababisha Halmashauri na Baraza la Madiwani kumchangia ili aweze kuanza masomo.


Akijibu hoja hizo, Ndg. Msonga amesema kuhusu upungufu wa madawati, walimu wakuu wanapaswa kuandaa maandiko rasmi na kufuata taratibu zilizowekwa ili benki iweze kupitia na kuona namna bora ya kushiriki katika kutatua changamoto hiyo. Kuhusu mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Kibaha, Meneja huyo amesisitiza kuwa taratibu za kuomba ufadhili zinapaswa kufuatwa kwa kujaza maombi kupitia mfumo wa mtandao kama itakavyoelekezwa rasmi.


Ameongeza kuwa Benki ya NMB ni mdau mkubwa wa Serikali katika kuunga mkono maendeleo ya nchi, ikichangia takribani asilimia 30.7 ya mapato, hali inayoonesha dhamira ya benki hiyo katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.


Mbali na ujumbe kuhusu gawio la TSh milioni 750, wataalamu wa NMB waliotembelea Halmashauri hiyo pia walitoa elimu kwa viongozi kuhusu masuala ya mikopo, uwekezaji na matumizi sahihi ya "credit card", ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo katika kuongeza uelewa wa kifedha kwa wadau wake.


Kwa ujumla, kikao hicho kimeonesha dhamira ya Benki ya NMB kuendelea kushirikiana na Serikali na Halmashauri za Wilaya katika kusukuma mbele maendeleo ya jamii na ustawi wa wananchi wa Wilaya ya Bariadi na Taifa kwa ujumla.


#NMB #NMBKwaJamii #Maendeleo #Elimu

Matangazo

  • TANGAZO LA UTEUZI WATENDAJI WA UCHAGUZI NGAZI YA VITUO October 22, 2025
  • TAARIFA YA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 February 19, 2024
  • KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI ZA MWAKA 2025 April 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WA UCHAGUZI MKUU 2025 October 15, 2025
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • NMB Yatangaza Gawio la TSh Milioni 750 Kurejesha kwa Jamii, Yaahidi Kuendelea Kusaidia Elimu na Afya Bariadi DC

    February 03, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI BARIADI DC LAPONGEZA UONGOZI WA HALMASHAURI KWA KULIPA MADENI YA WATUMISHI

    January 14, 2026
  • HALMASHAURI YA BARIADI YAENDELEA KUTEKELEZA MKATABA WA LISHE KWA UFAUJI MKUBWA

    November 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AKABIDHI TREKTA 26 KUANZA MSIMU MPYA WA KILIMO BARIADI

    October 13, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.

  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Togel
  • Situs Slot Gacor
  • Toto Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • KOI200
  • Slot Gacor
  • DORA77
  • Toto Slot
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • AXL777
  • AXL777
  • KOI200
  • KOI200
  • NABITOTO
  • NABITOTO
  • NABITOTO
  • NABITOTO
  • AERO88
  • AXL777
  • AXL777
  • DORA77
  • DORA77
  • Situs Toto
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • NABITOTO
  • KOI200
  • yamitoto
  • slot gacor
  • aero88
  • ufabet
  • ufabet
  • ufabet
  • ufabet
  • ufabet
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • Situs Toto
  • KOI200
  • Toto Slot Gacor
  • AERO88 Slot Gacor
  • Slot Gacor
  • Slot Gacor
  • AERO88
  • Situs Toto
  • situs toto
  • slot gacor
  • situs toto
  • yamitoto
  • kudetabet98
  • kudetabet98
  • yamitoto
  • dora77
  • koi200
  • aero88
  • yamitoto
  • axl777
  • dora77
  • dora77
  • aero88
  • aero88
  • dora77
  • dora77
  • slot gacor
  • axl777
  • axl777
  • yamitoto
  • axl777
  • axl777
  • axl777
  • axl777
  • axl777
  • axl777
  • yamitoto
  • axl777
  • aero88
  • dora77
  • yamitoto
  • dora77