• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

UIBUAJI MIRADI JAMII KUPITIA TASAF WAENDA KUTOA AJIRA ZA MUDA KWA WALENGWA

Posted on: September 3rd, 2024


Akifungua kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Kijiji cha Isenge, Kata ya Dutwa tarehe  28/08/2024, Mhandisi Emmanuel Sekwao kutoka Makao Makuu ya Ofisi za Tasaf, Dodoma akiwa  amefuatana na Wataalamu kutoka ofisi za Tasaf Dar es salaam, Morogogoro, Tanga na Halmashauri ya Mji Musoma, alisema lengo la kufika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ni kutaarifu maboresho ambayo  yamefanyika katika Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).


Mhandisi Emmanuel Sekwao, aliwaeleza wananchi wa kata ya Dutwa pamoja na Wataalamu wa halmashauri kuwa lengo kuu ni  kuwataarifu maboresha ambayo yamefanyika kwenye mfuko na kuwa maboresho hayo yatakuwa sehemu ya kujifunza Wataalamu wa halmashauri

kwa ajili ya zoezi ambalo liko mbele yao la Uibuaji Miradi Midogomidogo ambayo itatekelezwa na Walengwa wa Mpango wa TASAF.


" Tumezoea kuwa wale walengwa wetu wa mpango wa TASAF kuna malipo wanayoyapokea kila baada ya miezi miwili,mabadiliko ambayo yamefanyika, wale walengwa ambao wako kwenye mpango na Kaya zao zinaweza kutoa Nguvu Kazi wenye umri kati ya miaka 18-65 zitaingia kwenye utaratibu mpya wakufanya kazi ndogondogo ( Miradi ya Jamii). Watakavyokuwa wanatekeleza hizo kazi, watalipwa Ujira badala ya Ruzuku ile ya msingi .Kazi itafanywa kwa masaa manne kwa siku kumi katika mwezi mmoja, na mradi unapaswa kukamilika ndani ya miezi sita, hivyo mlengwa atafanya kazi siku sitini". Alisema Mhandisi.


Aidha alisema kazi hizo za miradi midogo zinafahamika pia kama ajira za muda, kabla ya mpango huo, mlengwa alikuwa

anapewa ruzuku ya msingi tsh. 144,000 Kwam mwaka lakini kwa sasa yule atakayekuwa kuwa ameandikishwa kwenye ajira ya mpango wa muda atalipwa tsh 180,000 kwa mwaka ikiwa ni maboresho yaliyofanyika.


Ruzuku  ambazo Kaya maskini zimekuwa zikipokea, ziligawiwa kakita makundi mawili, ruzuku za Msingi na ruzuku za Masharti,lakini kupitia mpango huu mpya wa Uibuaji Miradi ambao umewanufaisha walengwa katika maeneo mengine nchini,walengwa watapata ajira za muda zitakazowanufaisha kwa kukua kiuchumi na kupata miradi itakayowanufaisha jamii yote kwa pamoja.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.