• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

UJENZI WODI YA WATOTO HOSPITALI YA WILAYA KUKAMILIKA

Posted on: February 4th, 2025

Kamati ya Elimu, Afya na Maji ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, tarehe 22 Januari 2025, ilifanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa wodi ya watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Bariadi. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa miradi ya afya katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025.


Mganga Mfawidhi wa Wilaya, Ndg. Magembe Kuligwa Pelana, alibainisha kuwa kiasi cha Tsh 172,000,000 kilitolewa kwa hospitali hiyo kwa ajili ya kukamilisha Wodi Ya Watoto, Jengo la Upasuaji, na Jengo la kuhifadhi Maiti. Kati ya fedha hizo, Tsh 59,828,767 tayari zimetumika kwa wodi ya watoto.


Mradi huo, unaosimamiwa na mkandarasi, umefikia hatua za mwisho za ukamilishaji, ikiwa ni pamoja na kuunganisha mifumo ya maji safi, maji taka, umeme, na kufunga milango pamoja na madirisha ya vioo. Ujenzi unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo tarehe 2 Februari 2025, ambapo huduma kwa watoto zitaanza kutolewa.


Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Jonas Nyaena, alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa msaada mkubwa wa serikali katika kufanikisha miradi ya maendeleo. Pia aliwashukuru wataalamu wote kwa jitihada za kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana kwa jamii.


Katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imeidhinisha Tsh 472,000,000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa hospitali hiyo, hatua inayotoa matumaini makubwa kwa wakazi wa Wilaya ya Bariadi.


Ujenzi wa wodi ya watoto ni hatua muhimu katika kuboresha huduma za afya, hasa kwa watoto, na kuimarisha ustawi wa jamii kwa ujumla

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.