• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

UKAGUZI WA MRADI KITARU CHA MITI BARIADI DC

Posted on: January 23rd, 2025


Mnamo tarehe 23 Januari 2025, Kamati ya Uchumi, Ujenzi, na Mazingira ilifanya ukaguzi wa Mradi wa Kitalu cha Miti uliopo katika makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi. Mradi huu unaofadhiliwa na Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi wa Mkoa wa Simiyu (SCRP) pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, umefanikiwa kutokana na ushirikiano wa wadau mbalimbali.


Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Misitu Wilaya, Bi Bahati Pius, mradi huu umepokea ufadhili wa Tsh. 1,925,400/= kutoka SCRP kwa ajili ya ununuzi wa vifaa, na Tsh. 2,039,000/= kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa ajili ya shughuli za kujaza viriba, ununuzi wa mbegu, uvutaji wa maji, na huduma za kitalu. Hadi sasa, mradi umegharimu jumla ya Tsh. 3,964,400/=.


Shughuli za kuandaa kitalu zilianza tarehe 20 Oktoba 2024, zikilenga kuotesha miche 20,000 ya kivuli (19,250) na matunda (750). Licha ya changamoto kama mifugo kula miche na ukame, uotaji wa mbegu umefikia asilimia 90, jambo linalodhihirisha maendeleo mazuri ya mradi.


Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Duka Mashauri Mapya, alitoa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Halidi M. Mbwana, na wataalamu wote kwa juhudi zao. Tangu kuanza kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri imeweza kusambaza miche 204,458 kwa taasisi mbalimbali, zikiwemo shule na vituo vya afya.


Mradi huu unaonyesha umuhimu wa usimamizi bora na ushirikiano katika jitihada za hifadhi ya mazingira, huku ukiwa na mchango mkubwa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.