• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

Posted on: April 30th, 2025

Bariadi, Simiyu – Aprili 30, 2025:

Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi inatarajia kuanza kutoa dozi ya pili ya chanjo ya sindano ya polio (IPV2) kwa watoto kuanzia mwezi Mei 2025, kama hatua ya kuimarisha kinga dhidi ya ugonjwa wa kupooza kwa watoto walio katika hatari zaidi.


Hayo yamesemwa katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika tarehe 29 Aprili 2025 katika Makao Makuu ya Halmashauri hiyo. Akizungumza na wajumbe wa kikao hicho, Mratibu wa Chanjo Wilaya, Ndg. Abdulazizi Ramadhani, amesema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa polio katika nchi jirani zikiwemo Malawi, Zambia, Burundi na Congo.


"Kutokana na mwingiliano wa wananchi baina ya Tanzania na mataifa haya, kuna hatari ya maambukizi ya virusi vya polio. Chanjo hii ya pili inalenga kuongeza kinga kwa watoto walio na umri wa miezi tisa," alisema Ndg. Ramadhani.


Ameeleza kuwa ugonjwa wa polio unasababishwa na virusi vya Poliovirus vinavyoweza kuingia mwilini kupitia chakula au maji machafu, na baadaye kushambulia mishipa ya fahamu, hivyo kusababisha kupooza. Alibainisha kuwa dozi ya kwanza ya sindano ya polio (IPV) hutolewa mtoto anapofikisha wiki 14, na kwamba hii ni nyongeza ili kuimarisha kinga zaidi.


Katika kikao hicho, mmoja wa wazee maarufu kutoka Kijiji cha Igaganulwa, Bw. Amos M. Lubacha, alihoji kwa nini chanjo hiyo inalenga watoto pekee ikiwa ugonjwa huo ni hatari kwa wote. Akijibu swali hilo, Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Pilila Zambi, alieleza kuwa kwa sasa maelekezo ya Wizara ya Afya ni kutoa chanjo hiyo kwa watoto wa miezi tisa, na iwapo kutatokea mabadiliko, jamii itaelekezwa ipasavyo.


Kwa upande wake, Mgeni Rasmi wa kikao hicho ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Bariadi, Ndg. Justine Manko, amewataka wajumbe wote kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa chanjo na hasa kinga dhidi ya ugonjwa hatari wa polio.


Wajumbe wa kikao hicho walihusisha Kamati ya Usalama ya Wilaya, wazee maarufu, viongozi wa kijadi na dini pamoja na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.


Kwa mara ya mwisho Tanzania iliripoti mgonjwa wa polio mwaka 1996, lakini kutokana na tishio la kurudi kwa ugonjwa huo duniani, serikali imeamua kuimarisha kinga ili kuzuia uwezekano wa maambukizi nchini.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.