• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

Vijana Wachapakazi Banemhi Wafanikiwa Kupitia Mradi wa Bodaboda

Posted on: September 1st, 2025

Kikundi cha Vijana Wachapakazi kutoka Kijiji cha Banemhi, Kata ya Banemhi, kimeendelea kuonyesha mafanikio makubwa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2022.

Kikundi hiki chenye wanachama sita (wote wanaume) kilisajiliwa rasmi tarehe 28 Aprili 2022 kwa Namba CD/BRD/CBO/1006, na kimekuwa mfano wa utekelezaji bora wa mikopo ya vijana inayotolewa na Halmashauri kupitia Mfuko wa Vijana 4%.

Mradi huu, ambao ulizinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa tarehe 05 Agosti 2024 ukiongozwa na Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava, umegharimu jumla ya Tsh. milioni 20. Kati ya hizo, Tsh. milioni 2 zilitokana na mchango wa wanakikundi na Tsh. milioni 18 ni mkopo wa Halmashauri.

Ajira na Maendeleo ya Kijamii

Kupitia shughuli za usafirishaji (bodaboda), wanakikundi wote sita wamepata ajira ya kudumu, huku baadhi yao wakiweza kuboresha makazi na kushiriki katika huduma za kijamii ikiwemo elimu na afya. Aidha, mradi huu umehamasisha vijana wengine kuanzisha vikundi vya kiuchumi kupitia mikopo ya mapato ya ndani.

Marejesho ya Mkopo

Hadi sasa kikundi kimefanikiwa kurejesha Tsh. milioni 13.6 ndani ya mwaka mmoja, na kimesalia na deni la Tsh. milioni 4.4 pekee.

Mikakati ya Kuendeleza Mradi

Ili kuhakikisha mradi unakuwa endelevu, vijana hao wameweka mikakati ya kupata mafunzo ya ujasiriamali, kuanzisha mfumo wa kumbukumbu za mapato na matumizi, kutenga sehemu ya mapato kwa matengenezo na upanuzi wa mradi, pamoja na kuimarisha ushirikiano na Halmashauri kwa msaada wa kitaalamu.

Mfano wa Utekelezaji wa Sera za Serikali

Mradi wa Vijana Wachapakazi Banemhi unatajwa kuwa mfano bora wa utekelezaji wa sera za Serikali kupitia mikopo ya Mfuko wa Vijana (4%), inayolenga kuwawezesha vijana kujitegemea, kuongeza kipato na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii.


Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Vijana Wachapakazi Banemhi Wafanikiwa Kupitia Mradi wa Bodaboda

    September 01, 2025
  • Nigo Lodge – Nguzo ya Maendeleo Igaganulwa, Bariadi

    August 26, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.