• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

BARIADI DC YABAINISHA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA MWAKA 2024/2025

Posted on: December 17th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi leo tarehe 17 Disemba 2024 imewasilisha taarifa ya mapitio ya Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambayo imeeleza shughuli na miradi mbalimbali iliyotekelezwa katika kipindi cha nusu mwaka na inayoendelea kutekelezwa.

Akiwasilisha taarifa hiyo katika kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya (DCC) Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Ndg. Sayi Luseba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Bariadi alibainisha kuwa katika mwaka wa fedha 2024/2025 halmashauri ya wilaya ya Bariadi ilikisia kupata kiasi cha fedha Shilingi Bilioni 35.7 kutoka vyanzo mbalimbali kama vile mapato ya ndani shilingi bilioni 2.5 ruzuku toka serikali kuu (OC) bilioni 2.1 mishahara bilioni 22.9 na miradi ya maendeleo bilioni 8.

Miongoni mwa shughuli na miradi inayotekelezwa ni pamoja na kuchangia kiasi cha shilingi milioni 33.2 kwaajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 400 kwaajili ya jengo la upasuaji na wodi mbili za upasuaji katika hospitali ya Wilaya ya Bariadi. Kutoa fedha za ruzuku kwa kaya masikini 6,510 ambapo jumla ya shilingi milioni 953 zimelipwa kwa walengwa hao pamoja na ujenzi wa shule mpya mbili za sekondari kata ya Nkololo moja ikiwa ni shule ya amali ambapo kila mradi una thamani ya shilingi milioni 584.

Ndg. Luseba alieleza pia changamoto mbalimbali ambazo zinazojitokeza katika utekelezaji wa mpango na bajeti wa mwaka 2024/2025 ambapo moja ya changamoto hiyo ni matumizi ya fedha nyingi katika kudhibiti wanyama wa kali ambao huvamia vijiji vilivyopo kandokando ya hifadhi.

kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya Bariadi kiliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Simon Simalenga na kushirikisha wadau mbalimbali kama vile wakuu wa Idara na vitengo kutoka halmashauri ya mji na halmashauri ya wilaya ya Bariadi, viongozi wa taasisi za serikali, viongozi wa vyama vya siasa, watendaji wa kata pamoja na viongozi wa dini ambao kwa ujumla wao waliweza kutoa michango yao katika mapendekezo ya mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.