Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Simon Simalenga, tarehe 30/05/2025 amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya elimu, ikiwemo ujenzi wa bwalo la chakula katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Simiyu, pamoja na shule za sekondari Mwamoto, Ihusi na Amali.
Katika awamu ya pili ya utekelezaji wa mradi huu kupitia Programu ya SEQUIP (Secondary Education Quality Improvement Project), Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ilipokea fedha zifuatazo:
TSh. Bilioni 1.1 (iliyopokelewa tarehe 21 Juni 2024) kwa ajili ya ujenzi wa:
Vyumba 10 vya madarasa
Chumba cha maktaba
Chumba cha TEHAMA
Mabweni 4 ya wanafunzi
Vyumba 3 vya walimu
TSh. Milioni 350 (iliyopokelewa tarehe 22 Agosti 2024) kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa Bwalo la Chakula katika Shule ya Wasichana ya Mkoa.
Mhe. Simalenga amepongeza kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo na kueleza kuridhishwa kwake na hatua zilizofikiwa. Ameelekeza kuhakikisha kazi zote zilizobaki zinakamilika kwa wakati, ikiwemo umaliziaji wa ngazi za mbele ya bwalo hilo la chakula.
Ziara hiyo ni sehemu ya usimamizi shirikishi wa viongozi wa Serikali kuhakikisha kuwa rasilimali zilizotolewa zinatumika ipasavyo na miradi inatekelezwa kwa ubora na kwa wakati.
#SimiyuYajengwa
#BariadiInaendelea
#SEQUIP
#WasichanaElimuMsingi
#UwekezajiKwenyeElimu
#DCBariadi
#MkoaSimiyu
Bariadi
Anuani: 109-Bariadi
Simu: 028 2700012
Simu: +255683705815
Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz
Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.