• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

FZS YABORESHA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI NA KUGHARAMIA HATI MILKI 100 KWA MAKUNDI MAALUM WILAYANI BARIADI

Posted on: June 18th, 2025

Bariadi, Simiyu – Juni 10, 2025


Katika kuimarisha matumizi bora ya ardhi na kulinda ikolojia ya Serengeti, Shirika la Frankfurt Zoological Society (FZS) limefadhili upimaji na utoaji wa hati milki 100 za kimila kwa wananchi wa makundi maalumu katika vijiji 18 vinavyopakana na Hifadhi ya Serengeti, Pori la Akiba Kijereshi na Pori la Akiba la Maswa, wilayani Bariadi.


Akizungumza wakati wa kikao maalum kilichofanyika katika Kijiji cha Ihusi, Mjumbe wa Kamati ya Mipango ya Matumizi Bora ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bi. Lucia Sweetbert, alisema kuwa shughuli hiyo ni muendelezo wa utekelezaji wa mpango wa matumizi ya ardhi ulioanzishwa mwaka 2024, ikiwa ni pamoja na usimikaji wa vigingi katika maeneo mbalimbali ya kijiji.


Katika kikao hicho, Bi. Lucia alitoa utambulisho wa awamu ya pili ya mradi wa Serengeti Ecosystem Development and Conservation Project, unaotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Wananchi wa Ujerumani (KfW), TANAPA na FZS.


“Mwaka huu tutaendelea na usimikaji wa mabango ya matumizi ya ardhi yenye maelezo ya wajibu na katazo kwa kila eneo lililotengwa, sambamba na kupata majina ya wanavijiji 100 kutoka makundi maalum kwa ajili ya kupimiwa ardhi na kupewa hati milki za kimila bila gharama yoyote,” alisema Bi. Lucia.


Alifafanua kuwa wanufaika wa mpango huo ni wajane, walemavu, wazee, watu wenye kipato duni na wagane, ambapo watu 25 walichaguliwa mwaka 2018 na wengine 75 waliteuliwa kupitia mchakato wa mwaka 2024, wakiwakilisha vitongoji mbalimbali vilivyotoa wastani wa watu 20 kila kimoja.


Bi. Lucia aliongeza kuwa zoezi la usimikaji wa mabango linafuata matumizi yaliyopitishwa na mkutano wa hadhara, yakiwemo maeneo ya makazi, taasisi, malisho na hifadhi za mito.


Kwa mujibu wa takwimu, hadi sasa wananchi 6,369 kutoka vijiji vya wilaya ya Bariadi wamefaidika na upatikanaji wa hati milki za kimila (CCROs) kupitia ufadhili wa FZS. Hatua hiyo imesaidia kuimarisha usalama wa miliki za ardhi, kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori, pamoja na kuchochea uwekezaji wa kijamii na kiuchumi katika maeneo hayo.


Kwa ujumla, jitihada hizo zinaendelea kuweka msingi imara wa matumizi endelevu ya ardhi na uhifadhi wa mazingira kwa maslahi ya kizazi cha sasa na kijacho.



Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MATUKIO YA UPIMAJI ARDHI YAKIWASILISHA NEEMA MPYA KWA WAKAZI WA BARIADI

    June 23, 2025
  • MIPAKA ILIYOPIGWA MARUFUKU KUTOLEWA HATI MILIKI YABAINISWA RASMI

    June 23, 2025
  • SAFARI YA PAMOJA BARIADI

    June 21, 2025
  • Mkuu wa Wilaya Atoa Pongezi kwa Baraza la Madiwani Bariadi kwa Uadilifu na Uwajibikaji wa Hali ya Juu

    June 21, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.