• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI WILAYA CHAJADILI RASIMU YA BAJETI YA 2025/2026

Posted on: February 21st, 2025

KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI WILAYA CHAJADILI RASIMU YA BAJETI YA 2025/2026

Bariadi, 21 Februari 2025 – Kikao cha Kamati ya Ushauri Wilaya (DCC) kimefanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, kata ya Dutwa, kikiongozwa na Mkuu wa Wilaya, Mhe. Simon P. Simalenga, ambapo wajumbe walijadili rasimu ya bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.


Akifungua kikao hicho, Mhe. Simalenga alisema lengo kuu ni kujadili changamoto zilizopo wilayani na kuzitafutia ufumbuzi kupitia bajeti ijayo. Alisisitiza kuwa bajeti hiyo inalenga kuimarisha utawala bora, kuongeza ukusanyaji wa mapato, na kuwekeza kwenye miradi ya maendeleo.


Kwa mujibu wa Afisa Mipango wa Wilaya, Ndg. Raymond Kilindo, bajeti ya 2025/2026 imezingatia vipaumbele vya wilaya, ikiwemo elimu, afya, usimamizi wa fedha, na motisha kwa watumishi wa umma. Alieleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi inatarajia kukusanya na kutumia shilingi bilioni 34.732 kutoka vyanzo mbalimbali, ikiwemo:

Mapato ya ndani – shilingi bilioni 2.6

Ruzuku ya mishahara – shilingi bilioni 22.9

Ruzuku ya matumizi ya kawaida – shilingi bilioni 1 

Fedha za miradi ya maendeleo – shilingi bilioni 8 


Katika kikao hicho, Mjumbe,Ndg. Stephen Kashinje aliuliza kuhusu utaratibu mpya wa utoaji wa mikopo kwa wananchi. Akijibu swali hilo, Afisa Mipango wa Wilaya alieleza kuwa taratibu zote zimeshaainishwa kupitia vikao vya Halmashauri na Baraza la Madiwani mpaka ngazi ya kijiji. Alisema baadhi ya wananchi tayari wameshapata mikopo na kuelekeza wale wenye maswali zaidi wanaweza kufika Ofisi ya Maendeleo ya Jamii wilaya kwa maelezo ya kina.


Kikao hicho kilihitimishwa kwa mapendekezo mbalimbali ya kuboresha utekelezaji wa bajeti na kuhakikisha rasilimali zinatumika kwa ufanisi ili kuinua maendeleo ya Wilaya ya Bariadi.



Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.