• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Apongeza Kituo cha Mafunzo ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Mazingira Bariadi

Posted on: August 13th, 2025



Bariadi, 13 Agosti 2025 — Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa Kitaifa, Ndg. Ismail Ali Ussi, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kwa mradi wa kipekee wa Kituo cha Mafunzo ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Uhifadhi wa Mazingira kilichopo Kata ya Dutwa, akisema ni jambo la mfano wa kuigwa katika nchi.

"Naamini hii ndiyo itakuwa stori ya pekee kwenye vyombo vya habari siku ya leo, maana katika mikoa 22 tulikopitia hatujakutana na mambo kama tuliyoyaona hapa. Nakupongeza sana Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi," alisema Ndg. Ussi.

Kauli hiyo aliitoa wakati Mwenge wa Uhuru ulipopita kukagua mradi huo unaotekelezwa kupitia Mapato ya Ndani ya Halmashauri, ukiwa na thamani ya Shilingi milioni 53.3

Historia na Lengo la Kituo

Akizungumza mbele ya kiongozi huyo wa Mwenge, Afisa Kilimo wa Wilaya, Ndg. Salim Hamad, alisema Kituo cha Rasilimali za Kilimo cha Bariadi kilianzishwa mwaka 2012 na kuhuishwa mwaka 2022, kikiwa na lengo la:

  • Kutoa mafunzo na elimu kwa wakulima na wafugaji juu ya teknolojia na mbinu bora za uzalishaji.
  • Kutoa huduma za ushauri na kufanya tafiti za kilimo, mifugo, uvuvi na uhifadhi wa mazingira.
  • Kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na uhifadhi wa mazingira.

Kituo kina jumla ya ekari 10, ambapo kwa sasa ekari 4.5 ndizo zinazotumika kikamilifu.

Shughuli Zinazotekelezwa

Kituo kimekuwa kikitekeleza shughuli mbalimbali ikiwemo:

  • Uzalishaji wa mazao kama mikunde, nafaka, mazao ya mafuta na mbogamboga.
  • Ufugaji wa mbuzi, kondoo, ndege wa aina mbalimbali na samaki aina ya sato.
  • Uzalishaji wa miche ya miti zaidi ya 72,253, ikiwemo ya matunda, kivuli, dawa na mbao.

Manufaa kwa Jamii

Miongoni mwa faida za mradi huu ni:

  • Kuwajengea uwezo wakulima na wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
  • Kuendeleza ufugaji wa kibiashara.
  • Kuhamasisha jamii kuhifadhi mazingira na kutumia nishati safi.

Shukrani kwa Uongozi wa Taifa

Halmashauri imetoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na uhifadhi wa mazingira, hususan kupitia masharti ya Ibara ya 9C(i) na (ii) na Ibara ya 253(j) ya Ilani ya CCM.

"Tunaahidi kuulinda na kuutunza mradi huu ili uendelee kuwasaidia wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kama ilivyokusudiwa," ilisisitiza uongozi wa kituo.


Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Vijana Wachapakazi Banemhi Wafanikiwa Kupitia Mradi wa Bodaboda

    September 01, 2025
  • Nigo Lodge – Nguzo ya Maendeleo Igaganulwa, Bariadi

    August 26, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.