Bariadi, Mei 29, 2025 – Maafisa Elimu Kata pamoja na Wakuu wa Shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi wamepatiwa mafunzo ya usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji fanisi kupitia jumuiya za kujifunza za walimu wakuu na maafisa elimu kata.
Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mwl. Hamisi Shololo, ambaye aliwataka washiriki kuyazingatia mafunzo hayo kwa umakini ili kuongeza ufanisi katika usimamizi wa elimu na hatimaye kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule zao.
> "Ninyi kama wasimamizi wa elimu katika maeneo yenu, naomba mambo mtakayofundishwa katika mafunzo haya yaweze kuwafikia walimu wote katika maeneo yenu, na tija ya mafunzo haya iweze kuonekana," alisisitiza Mwl. Shololo.
Mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Shule Bora, unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (UKAID). Mradi huu unatekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara, ikiwemo Mkoa wa Simiyu, kwa lengo la kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa watoto wote.
Bariadi
Anuani: 109-Bariadi
Simu: 028 2700012
Simu: +255683705815
Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz
Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.