Maafisa Habari kutoka Mikoa na Halmashauri za Simiyu na Shinyanga leo wameungana na Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, katika kikao kazi maalum kilichofanyika jijini Dodoma kwa ajili ya Maafisa Habari wa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs).
Kikao hicho cha siku mbili kilichoanza Mei 23, 2025, kililenga kutoa maelekezo na mwelekeo wa Serikali kuhusu namna bora ya kuhabarisha umma juu ya kazi na mafanikio ya Serikali, hasa kupitia taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI kama DART, TARURA, TSC, Shirika la Elimu Kibaha na Chuo cha Serikali za Mitaa – Hombolo.
Mhe. Mchengerwa amesisitiza umuhimu wa Maafisa Habari kuwa wabunifu na makini katika kusambaza taarifa sahihi, kwa wakati na kwa njia rafiki ili wananchi wafahamu kwa kina maendeleo yanayotekelezwa na Serikali yao.
Kikao hicho kimehitimishwa leo Mei 24, 2025 kwa ziara ya pamoja ya Maafisa Habari kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ili kujionea maendeleo ya miundombinu na huduma zinazotolewa.
Bariadi
Anuani: 109-Bariadi
Simu: 028 2700012
Simu: +255683705815
Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz
Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.