• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

MADIWANI WA BARIADI WAJIFUNZA UTALII WA NDANI HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Posted on: April 19th, 2025


Alfajiri na mapema, tarehe 17, Aprili 2025, Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi walianza safari yao maalum ya kujifunza na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukuza utalii wa ndani. Safari hiyo ilielekezwa katika Hifadhi maarufu ya Taifa ya Serengeti kupitia Lango la Ikoma, Wilaya ya Serengeti, Mkoa wa Mara.

Msafara huo uliongozwa na Muongozaji wa Hifadhi ya Serengeti, Ndg. Sebastian Elias, ambaye aliwakaribisha madiwani hao kwa kuwatambulisha  uzuri wa hifadhi hiyo maarufu duniani.


Ndg. Elias alieleza kuwa Serengeti ni moja ya maajabu ya dunia, inayojulikana kwa mandhari yake ya kuvutia ya savanna pana, miti ya akasia, na miamba ya asili maarufu kama kopjes ambayo wanyama hupanda kwa ajili ya kupumzika au kuotea mawindo.


Aliendelea kufafanua kuwa Serengeti ni makazi ya wanyama mbalimbali kama simba, tembo, chui, faru na duma, huku tukio la kipekee la 'The Great Migration' uhamaji mkubwa wa mamilioni ya nyumbu, pundamilia, na swala  likiwa moja ya vivutio vikubwa zaidi duniani.


Mhe. Duka Mashauri Mapya diwani Kata ya Mwadobana ,alisema kuwa fursa hiyo ya kushiriki katika utalii wa ndani imewasaidia kufahamu zaidi kuhusu thamani ya hifadhi hiyo kubwa.

Alibainisha kuwa Hifadhi ya Serengeti inajivunia ukubwa wa takribani kilomita za mraba 14,763, na hivyo kuwa moja ya maeneo makubwa zaidi ya uhifadhi wa wanyamapori barani Afrika.


Serengeti, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia uliotangazwa na UNESCO, inaendelea kuwa kivutio kikubwa cha utalii wa picha, tafiti za wanyamapori, na juhudi za uhifadhi wa mazingira.


Kwa ujumla, safari hiyo imetoa mwanga mpya kwa viongozi wa Wilaya ya Bariadi juu ya umuhimu wa kuhifadhi maliasili na kukuza utalii wa ndani kama sehemu ya maendeleo endelevu ya taifa.

https://www.instagram.com/p/DInv5ZisOfQ/?igsh=MWZ5cTM2amFtMWhreg==

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.