• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

MIFUGO 326,000 YACHANJWA NA KUTAMBULIWA NCHINI

Posted on: July 5th, 2025

Simiyu, Julai 5, 2025

Takribani mifugo 326,000 tayari imechanjwa na kutambuliwa nchini tangu kuanza kwa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo tarehe 2 Julai 2025.


Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa kampeni hiyo katika Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema hatua hiyo ni ishara ya dhamira ya Serikali katika kuboresha afya ya mifugo na kuinua thamani ya mazao yake kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.


“Tayari tumefikia hatua nzuri. Tumeanza kuchanja na kutambua mifugo yetu, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuimarisha afya ya mifugo na kuvutia masoko ya kimataifa. Pia, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alishatuletea madume bora 754 yaliyosambazwa kwa wafugaji nchi nzima. Leo hii tunatekeleza haya yote huku Serikali ikigharamia utambuzi kwa kutumia hereni za kielektroniki,” alisema Mhe. Dkt. Kijaji.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kiwanda cha kuchakata nyama cha Union Meat, Bi. Ng’hwani, alisema kuwa kampeni hiyo imeongeza thamani ya nyama wanayosindika na kuongeza uaminifu wa bidhaa hiyo katika masoko ya kimataifa.


“Mimi nilikuwa Jaji nchini Ushelisheli, lakini mazingira rafiki ya uwekezaji kwenye sekta ya mifugo niliyoyaona chini ya uongozi wa Rais Samia yamenisukuma kurudi na kuwekeza hapa nchini. Kupitia kampeni hii, tayari thamani ya nyama tunayozalisha imeanza kuonekana,” alieleza Bi. Ng’hwani.


Kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo ilizinduliwa rasmi tarehe 16 Juni 2025 katika Wilaya ya Bariadi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ziara ya Waziri Kijaji inalenga kufuatilia utekelezaji wa kampeni hiyo na inatarajiwa kuendelea katika mikoa ya Geita, Pwani, Morogoro, Tabora na Dodoma.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MRADI Wa MAJI BANHEMI WAKAMILIKA KWA MAFANIKIO!

    July 11, 2025
  • ‎UJENZI WA DARAJA LA MRIDAMRIDA – KATA YA NKINDWABIYE ‎

    July 10, 2025
  • UJENZI WA MIUNDOMBINU YA KUDHIBITI TAKA HATARISHI WAKAMILIKA KIKAMILIFU

    July 10, 2025
  • MIFUGO 326,000 YACHANJWA NA KUTAMBULIWA NCHINI

    July 05, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.