• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

Mkuu wa Wilaya Atoa Pongezi kwa Baraza la Madiwani Bariadi kwa Uadilifu na Uwajibikaji wa Hali ya Juu

Posted on: June 21st, 2025

Bariadi, Juni 20, 2025

Akifungua kikao kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Simon Simalenga, ametoa pongezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kwa kupata hati safi katika ukaguzi wa hesabu za mwaka wa fedha 2023/2024.


Mhe. Simalenga alianza kwa kumshukuru Mungu kwa afya njema na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.


"Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, nawapongeza kwa kufuata sheria na kuendelea kuwajibika katika matumizi ya rasilimali za umma," alisema Mhe. Simalenga.


Akitambua kuwa kikao hicho kimefanyika ikiwa ni siku ya mwisho ya utendaji wa Baraza la Madiwani nchini, Mhe. Simalenga aliwapongeza madiwani na watendaji wote wa Halmashauri kwa nidhamu, uadilifu, na ushirikiano wa hali ya juu alioupata katika kipindi chote cha utumishi wake.


"Ni jambo la ajabu na la kuigwa – mradi unakamilika, fedha inabaki, na mtendaji anatoa taarifa mwenyewe kwa Mkurugenzi. Hili si jambo la kawaida, ni watu wa kipekee," alisisitiza.


Aidha, aliwapongeza kwa maandalizi na usimamizi bora wa ziara ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyodumu kwa siku tano, ambayo ilimfurahisha na kumgusa Mhe. Rais mwenyewe.


Katika hotuba yake ya kufunga, alieleza fahari ya Mkoa wa Simiyu kwa mafanikio ya kielimu yanayotokana na uongozi thabiti wa baraza hilo, ambalo limefanikisha Mkoa kuwa miongoni mwa mikoa mitano bora kitaifa.


"Nawatakia kila la heri katika baraza lijalo, ambapo miradi na fedha za utekelezaji zitazidi kuongezeka kwani Bariadi DC inakwenda kusimamia jimbo kiutendaji," alihitimisha.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MATUKIO YA UPIMAJI ARDHI YAKIWASILISHA NEEMA MPYA KWA WAKAZI WA BARIADI

    June 23, 2025
  • MIPAKA ILIYOPIGWA MARUFUKU KUTOLEWA HATI MILIKI YABAINISWA RASMI

    June 23, 2025
  • SAFARI YA PAMOJA BARIADI

    June 21, 2025
  • Mkuu wa Wilaya Atoa Pongezi kwa Baraza la Madiwani Bariadi kwa Uadilifu na Uwajibikaji wa Hali ya Juu

    June 21, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.