• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bariadi Vijijini Aweka Wazi Ratiba ya Uchaguzi Mkuu 2025

Posted on: August 7th, 2025

Bariadi, 07 Agosti 2025 –
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bariadi Vijijini, Bi. Beatrice Gwamagobe, leo tarehe 07 Agosti 2025 ameongoza kikao muhimu kilichowakutanisha Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wadau wa Uchaguzi, na Asasi za Kiraia kwa lengo la kuweka wazi ratiba na hatua muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025.

Akifungua kikao hicho kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Bi. Gwamagobe alieleza kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetoa maelekezo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi kuwasilisha kwa wadau taarifa rasmi kuhusu kalenda ya uchaguzi ili kuhakikisha maandalizi yanafanyika kwa uwazi na kwa mujibu wa sheria.

Ratiba ya Utoaji Fomu za Uteuzi

Kwa mujibu wa ratiba iliyowasilishwa:

  • Zoezi la kuchukua na kurejesha fomu za uteuzi kwa wagombea wa nafasi ya Ubunge na Udiwani litaanza tarehe 14 hadi 27 Agosti 2025.
  • Wagombea wa ubunge watachukua na kurejesha fomu hizo katika Ofisi za Msimamizi wa Uchaguzi za Majimbo husika.
  • Wagombea wa nafasi za udiwani watafanya hivyo katika Ofisi za Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa ngazi ya Kata.
  • Zoezi hili litadumu kwa siku 14 mfululizo.

Siku ya Uteuzi wa Wagombea

Bi. Gwamagobe alifafanua kuwa tarehe 27 Agosti 2025 imetengwa rasmi kuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa nafasi za Rais na Makamu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Uteuzi huo utafanyika kwa siku moja na kukamilika ndani ya muda uliopangwa kisheria.

Kipindi cha Kampeni

  • Kampeni za uchaguzi kwa upande wa Tanzania Bara zitaanza tarehe 28 Agosti hadi 28 Oktoba 2025, kipindi cha siku 62.
  • Kwa upande wa Tanzania Zanzibar, kampeni zitaendeshwa kuanzia 28 Agosti hadi 27 Oktoba 2025, ikiwa ni siku 61, ili kuruhusu upigaji kura mapema.

Siku ya Upigaji Kura

Bi. Gwamagobe alithibitisha kuwa siku ya kupiga kura kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani itakuwa Jumatano, tarehe 29 Oktoba 2025.

Idadi ya Wapiga Kura Waliosajiliwa

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Tume, hadi sasa wapiga kura waliokwisha jiandikisha ni 37,655,559 kote nchini, ambao wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo wa kihistoria.

Mwisho

Kwa maelezo zaidi kuhusu kalenda ya uchaguzi na taratibu za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, tembelea tovuti rasmi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi www.nec.go.tz


Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Vijana Wachapakazi Banemhi Wafanikiwa Kupitia Mradi wa Bodaboda

    September 01, 2025
  • Nigo Lodge – Nguzo ya Maendeleo Igaganulwa, Bariadi

    August 26, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • MRADI WA MAJI SAPIWI WAZINDULIWA RASMI NA MWENGE WA UHURU 2025

    August 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.