• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

RC SIMIYU AANZA ZIARA BARIADI DC KIJIJI KWA KIJIJI

Posted on: January 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Kenani Kihongosi leo Januari 09, 2025 ameanza ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Kijiji kwa kijiji ambapo kwa kuanzia ameanza Kata ya Sapiwi vijiji vya Nyamikoma, Sapiwi, Mwandama, Igegu Magharibi na Igegu kisha kumalizia Kata ya Dutwa Kijiji cha Mwamabu.


Ziara hiyo yenye lengo la kusikiliza kero na changamoto za wananchi kisha kuzipatia ufumbuzi imekuwa na umuhimu mkubwa kwa wananchi kwani miongoni mwa changamoto zilizowasilishwa katika maeneo mengi ni changamoto ya ubovu wa barabara, changamoto ya uvamizi wa wanyamapori, changamoto ya maji na changamoto ya umeme.


Baada ya changamoto hizo kuwasilishwa Mhe.Kihongosi alizipatia ufumbuzi kupitia jopo la wataalamu kutoka Idara na taasisi mbalimbali za Serikali ambapo changamoto nyingi zilipatiwa majibu papo hapo na chache zilihitaji muda katika utatuzi wake.


"Lengo langu Mkuu wa Mkoa kuja hapa pamoja na viongozi wengine moja tujue wananchi wetu wanachangamoto gani, wananchi wetu wana kero zipi, na Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kwamba 'ninawatuma muende mukaniwakilishe, wajibu wenu ni kwenda kutatua na kumaliza kero za watu' ndio maana nimefika hapa, na hii ziara nitatembelea vijiji vyote 478 vya Mkoa huu na tutavimaliza kama ambavyo tulianza kutembelea kwenye Kata". Alisisitiza Mhe.Kihongosi


Aidha katika ziara yake miongoni mwa masuala ambayo ameyasisitiza ni pamoja na kudumisha amani na mshikamano huku akiwasihi wananchi kutokubali kugawanyika kwa sababu za kisiasa.


Ziara ya Mhe.Kihongosi kutembelea kila kijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi itaendelea siku ya kesho tarehe 10 Januari 2025 huku wananchi wakiombwa kujitokeza kwa wingi ili kuwasilisha kero na changamoto zinazowakabili.


Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • Muonekano Halisi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu

    May 31, 2025
  • ZIARA YA MIRADI YA MAENDELEO BARIADI DC

    May 30, 2025
  • Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Wapatiwa Mafunzo ya Usimamizi wa Ufundishaji na Ujifunzaji Fanisi.

    May 30, 2025
  • DC BARIADI AONYA WANANCHI KUTOCHUNGIA MIFUGO KWENYE MAPORI YA AKIBA

    May 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.