• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

RUWASA SIMIYU YATIA SAINI MIKATABA YA UJENZI WA MIRADI YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: January 11th, 2023

Wakala wa maji na Usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu imetia saini mikataba ya ujenzi wa miradi ya maji inayotarajiwa kutekelezwa kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023.

Akieleza katika Hafla fupi ya utiaji saini Meneja wa RUWASA mkoa wa Simiyu Mhandisi Mariam Majala amebainisha kuwa kwa mwaka huu wa fedha wanatarajia kutekeleza miradi 15 ya maji bomba ikiwa miradi 10 kati ya hiyo itatekelezwa Wilaya ya Bariadi, mradi 1 wilaya ya Busega, mradi 1 wilaya ya Itilima, miradi 2 wilaya ya Maswa na mradi 1 wilaya ya Meatu.

Vilevile RUWASA mkoa wa Simiyu inatarajia kuchimba visima virefu 28, Wilaya ya Bariadi visima 10, wilaya ya Itilima visima 4, Wilaya ya  Maswa visima 10 na Wilaya ya Meatu visima 4. Pia inatarajia kufanya ukarabati wa Pampu za mkono 370.

Meneja huyo alifafanua kuwa miradi hiyo ipo katika hatua za mwisho za manunuzi na tayari mikataba ya ujenzi wa miradi 8 imekamilika na utiaji saini ndio umefanyika leo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh.Dokt. Yahaya Nawanda ambaye alishuhudia utiaji saini huo licha ya kutoa Shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dokt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo lakini aliwataka wakandarasi wote watakaotekeleza miradi hiyo kutekeleza kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa, aidha Mh. Nawanda aliwasisitiza kuwa Viongozi wa Mkoa na Wilaya hawatamvumilia mkandarasi yeyote atakayetekeleza miradi hiyo chini ya kiwango au kuchelewesha.

“Sisi Mkoa wetu tunataka miradi mizuri, tunataka tusimamie fedha za serikali vizuri ili mwisho wa siku wananchi wanufaike na fedha zao” alisisitiza Dokt. Nawanda

Miongoni mwa miradi inayotarajiwa kutekelezwa katika mwaka huu wa fedha Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ni miongoni mwa Halmashauri zitakazonufaika na miradi hiyo ambapo kata za Ngulyati, Sakwe, Mwadobana, Sapiwi, Mwaubingi na Matongo zinatarajia kupata miradi.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA WATENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 24, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA WATENDAJI WA VIJIJI February 23, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 - BARIADI DC December 14, 2022
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MKOA WA SIMIYU WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI

    May 19, 2023
  • DC BARIADI AFANYA KIKAO NA VIKOSI KAZI VYA PAMBA VYA KATA ZOTE

    May 11, 2023
  • WADAU KUTOKA KATA 09 ZA BARIADI DC WAJENGEWA UWEZO JUU YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST

    May 02, 2023
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YATEMBELEA MIRADI YA JOSHO NA KIKUNDI CHA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

    April 13, 2023
  • Angalia Vyote

Video

Ukamilishaji wa Shughuli za Madawati
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255712431642

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.