• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

RUWASA SIMIYU YATIA SAINI MIKATABA YA UJENZI WA MIRADI YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: January 11th, 2023

Wakala wa maji na Usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu imetia saini mikataba ya ujenzi wa miradi ya maji inayotarajiwa kutekelezwa kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023.

Akieleza katika Hafla fupi ya utiaji saini Meneja wa RUWASA mkoa wa Simiyu Mhandisi Mariam Majala amebainisha kuwa kwa mwaka huu wa fedha wanatarajia kutekeleza miradi 15 ya maji bomba ikiwa miradi 10 kati ya hiyo itatekelezwa Wilaya ya Bariadi, mradi 1 wilaya ya Busega, mradi 1 wilaya ya Itilima, miradi 2 wilaya ya Maswa na mradi 1 wilaya ya Meatu.

Vilevile RUWASA mkoa wa Simiyu inatarajia kuchimba visima virefu 28, Wilaya ya Bariadi visima 10, wilaya ya Itilima visima 4, Wilaya ya  Maswa visima 10 na Wilaya ya Meatu visima 4. Pia inatarajia kufanya ukarabati wa Pampu za mkono 370.

Meneja huyo alifafanua kuwa miradi hiyo ipo katika hatua za mwisho za manunuzi na tayari mikataba ya ujenzi wa miradi 8 imekamilika na utiaji saini ndio umefanyika leo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh.Dokt. Yahaya Nawanda ambaye alishuhudia utiaji saini huo licha ya kutoa Shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dokt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo lakini aliwataka wakandarasi wote watakaotekeleza miradi hiyo kutekeleza kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa, aidha Mh. Nawanda aliwasisitiza kuwa Viongozi wa Mkoa na Wilaya hawatamvumilia mkandarasi yeyote atakayetekeleza miradi hiyo chini ya kiwango au kuchelewesha.

“Sisi Mkoa wetu tunataka miradi mizuri, tunataka tusimamie fedha za serikali vizuri ili mwisho wa siku wananchi wanufaike na fedha zao” alisisitiza Dokt. Nawanda

Miongoni mwa miradi inayotarajiwa kutekelezwa katika mwaka huu wa fedha Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ni miongoni mwa Halmashauri zitakazonufaika na miradi hiyo ambapo kata za Ngulyati, Sakwe, Mwadobana, Sapiwi, Mwaubingi na Matongo zinatarajia kupata miradi.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.