• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

WATAALAMU BARIADI DC WAPATIWA MAFUNZO YA UBIA KATI YA SEKTA YA UMMA NA SEKTA BINAFSI

Posted on: February 13th, 2025


Wataalamu wa Kamati ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi wamepatiwa mafunzo kuhusu namna ya kuandaa miradi kwa mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). Mafunzo hayo yalitolewa jana, Februari 13, 2025, na wawakilishi kutoka Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), wakiongozwa na Dr. Edward Makoye na Ndg. Jones Mwalemba.


Lengo la mafunzo hayo lilikuwa kuwaelimisha wataalamu wa Halmashauri juu ya miongozo mbalimbali ya ufadhili wa miradi ya maendeleo kwa kushirikiana na sekta binafsi. Akizungumza katika mafunzo hayo, Dr. Edward Makoye alieleza kuwa sekta binafsi inaweza kushiriki katika utekelezaji wa majukumu ya serikali kwa njia mbalimbali, zikiwemo ujenzi wa miundombinu mipya na kuiendesha kwa niaba ya serikali,utoaji wa huduma kwa kutumia miundombinu ya serikali iliyopo na ukarabati pamoja na uendeshaji wa miundombinu ya serikali kupitia makubaliano maalum.


Katika mafunzo hayo, Dr. Makoye alitaja miradi kadhaa inayotekelezwa kwa mfumo wa PPP, ikiwemo Expressway ya Tozo kutoka Kibaha hadi Dodoma, Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi (DART) awamu ya 1-6, na ukarabati wa miundombinu ya reli ya TAZARA.


Kwa mujibu wa sheria ya PPP, miradi inaweza kutekelezwa kupitia njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na serikali kuibua na kuandaa miradi kabla ya kushirikisha sekta binafsi, mwekezaji binafsi kuibua mradi na kugharamia andiko lake kwa ajili ya kutekelezwa kwa ubia na serikali, majadiliano ya moja kwa moja kati ya serikali na mwekezaji binafsi mwenye sifa zinazokidhi vigezo vya mradi husika na pia serikali inaweza kushirikiana na sekta binafsi katika miradi iliyoibuliwa, ambapo uidhinishaji wake hufanywa na Baraza la Mawaziri baada ya kupokea ushauri kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.


Mafunzo hayo pia yalitoa fursa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kuwasilisha miradi yao inayopangwa kutekelezwa kwa mfumo wa PPP. Mkuu wa Kitengo cha Mipango Wilaya, Ndg. Raymond Kilindo, alibainisha kuwa Halmashauri tayari imeandaa maandiko kwa ajili ya miradi sita, ambapo miradi minne imechaguliwa kwa utekelezaji wa awali. Kwa sasa, taratibu za kuandaa maandiko kwa ajili ya utekelezaji wake zimeanza kwa kushirikiana na wataalamu kutoka PPPC.


Akizungumzia umuhimu wa PPP, Dr. Makoye alisema kuwa ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi unaleta faida nyingi, zikiwemo kuongeza ujuzi na ubunifu hasa katika teknolojia, kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma, kuongeza rasilimali fedha, na kuhakikisha mali za serikali zinatunzwa ipasavyo.


Mafunzo hayo yameleta mwanga kwa wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi juu ya fursa zilizopo katika mfumo wa PPP, huku matarajio yakiwa ni kutekeleza miradi ya maendeleo kwa njia bora zaidi kwa manufaa ya wananchi.



Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.