• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

‎WATUMISHI WAPYA BARIADI WAELIMISHWA KUHUSU MAADILI NA UWAJIBIKAJI KAZINI ‎

Posted on: July 16th, 2025

‎Bariadi, 16 Julai 2025 – Watumishi wapya wa umma, wengi wao wakiwa ni walimu pamoja na watumishi kutoka idara mbalimbali, leo wamepatiwa semina kuhusu Maadili ya Utumishi wa Umma na Uwajibikaji kazini. Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.

‎

‎Akizungumza wakati wa semina hiyo, Kaimu Katibu Msaidizi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Wilaya ya Bariadi, Ndg. Wang’engi M. Mohabe, alieleza kuwa ili mwalimu athibitishwe kazini ni lazima awe amemudu majukumu yake kikamilifu katika kipindi cha matazamio.

‎

‎“Baada ya tathmini ya utendaji wa mwalimu katika kipindi cha miezi 12, Katibu Msaidizi huwasilisha mapendekezo ya mwajiri kwenye kikao cha Kamati ya Wilaya ambayo huamua kama mwalimu athibitishwe, apewe muda zaidi wa kujirekebisha au ajira yake isitishwe,” alisema Mohabe.

‎

‎Aidha, alibainisha kuwa sifa zinazozingatiwa katika upandishaji wa cheo kwa mwalimu ni pamoja na utendaji bora wa kazi, kiwango cha elimu, muundo wa kada, nafasi ya kazi, cheo cha awali, bajeti ya mwajiri na idadi ya watumishi (ikama) iliyoidhinishwa.

‎

‎Kuhusu masuala ya kinidhamu, Mohabe alifafanua kuwa Wakuu wa Shule ni mamlaka ya kwanza ya kinidhamu kwa walimu katika ngazi ya shule, huku Tume ya Utumishi wa Walimu ngazi ya Wilaya ikiwa ni mamlaka ya rufaa kwa walimu wasioridhika na maamuzi hayo.

‎

‎“Walimu wanaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa makosa kama vile utoro wa siku tano mfululizo, wizi, ubadhirifu wa mali za umma, kuchelewa kazini, matumizi mabaya ya rasilimali, ugomvi kazini, uchonganishi, ulevi, na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi,” alisisitiza.

‎

‎Kwa upande wake, Afisa Utumishi wa Wilaya ya Bariadi, Ndg. Hassan Malingumu, aliwaeleza washiriki kuhusu haki za msingi za watumishi wa umma, ikiwa ni pamoja na kulipwa mshahara, posho ya kujikimu, fidia endapo kuna ajali au kifo kazini, uhamisho na likizo.

‎

‎Semina hiyo iliandaliwa kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi hao wapya kuhusu wajibu, haki, na mipaka yao katika utumishi wa umma. Mada mbalimbali ziliwasilishwa na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo TSC, Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Uthibiti Ubora wa Elimu na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.

‎

‎Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Bariadi, katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2025, Halmashauri ilipokea Kibali Na. FA.97/288/01/09 cha tarehe 25 Juni 2025, cha kupangiwa watumishi kutoka kada mbalimbali. Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2025, jumla ya watumishi wapya 45 walikuwa wameripoti kazini, huku taratibu za kiutumishi zikiendelea.

‎

‎

‎

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • ‎WATUMISHI WAPYA BARIADI WAELIMISHWA KUHUSU MAADILI NA UWAJIBIKAJI KAZINI ‎

    July 16, 2025
  • ‎FURAHA YA KUSOMA – MAKTABA YA KISASA YANG’ARA NKOLOLO SEKONDARI

    July 16, 2025
  • ‎‎ ‎ MRADI WA KITALU CHA MICHE 50,000 – Bariadi DC

    July 12, 2025
  • MRADI Wa MAJI BANHEMI WAKAMILIKA KWA MAFANIKIO!

    July 11, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.