• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Bariadi District Council
Bariadi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi

  • Mwanzo
  • Huduma
    • Elimu
    • Teknolojia Habari na Mawasiliano
    • Maji
    • Miundombinu
    • Mapato
      • Mazao
      • Pamba
      • Zabuni
      • Minada
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Formu za Maombi
    • Bajeti
    • Vibali
    • Miungozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albamu za Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Endelevu
    • Uwekezaji

ZAIDI YA BILIONI 20 ZITABADILISHA MAKAZI YA WATU KATA YA SAPIWI, MKOA WA SIMIYU.

Posted on: June 11th, 2024


Chuo  Kikuu cha Usimamizi wa Fedha,kata ya Sapiwi, mkoa wa Simiyu ni moja kati ya vyuo vitakavyonufaika na mikopo kutoka Benki ya Dunia kupitia miradi ya kuendeleza vyuo vikuu nchini ( Higher Education Economic Transformation Project, HEET Projects). Mkopo huo  unalenga kukipanua chuo kwa kujenga majengo ya kisasa chini ya usimamizi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia, na hata kusababisha ongezeko la wanafunzi.


Akiongea na menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi tarehe 10/6/2024 ndani ya ukumbi mkubwa wa halmashauri, Mkurugenzi wa kampasi ya chuo hicho, Ndg Ibrahim R. Kikwiye amesema halmashauri ya wilaya ikiwa ni moja ya  wanufaika wametembelewa na wageni kutoka Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Tekinolojia na mwakilishi wa Benki ya Dunia. Lengo la ugeni huo ni kuja kuhamasisha wananchi wa Simiyu hasa wale ambao wako karibu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha waelewe kuwa kutakuwa na fursa zitakazopatikana baada ya ujenzi wa chuo kupanuka na kusababisha ongezeko la wanafunzi.Kama inavyojulikana serikali pekee haiwezi kuleta mafanikio, watu binafsi wanapaswa kuhusishwa ili nao waweze kuwekeza katika sekta tofauti ikiwemo biashara ili mji uendelee (PUBLIC PRIVATE PARTNERSHIP, PPP). Wananchi wanapaswa kuona fursa zitakazopatikana katika mradi huo wa kujenga Chuo Kikuu.


Akifafanua zaidi amesema dola milioni 10.56 ambazo ni mkopo wa bei nafuu uliopatikana kutoka Benki ya Dunia, ndio mgao uliopatikana kwa ajili ya kuendelea Chuo cha Usimamizi wa Fedha. Ameeleza matumizi ya fedha hizo yamegawanyika katika maeneo saba na eneo kubwa lililopata mkopo zaidi ya 80% ni kampasi ya Sapiwi, mkoa wa Simiyu ambacho ni kiasi cha dola za kimarekani 8.5 ambazo ni sawa na bilioni 22 kwa ajili ya ujenzi. Kati ya hizo asilimia kidogo itaenda kwa ajili ya ujenzi wa kampasi ya Mwanza na zaidi ya bilioni 20 zitajenga kampasi ya Simiyu. Pesa hizo zitatumika kujenga jengo la madarasa, ghorofa 3 ambazo ndani yake kutakuwa na ofisi za walimu, ofisi nyingine na chumba cha mapumziko. Ujenzi mwingine ni majengo 2 yenye ghorofa moja yatakayotumika kama mabweni, na kila bweni litachukuwa wanafunzi 150. Kutakuwa na jengo  kwa ajili ya maktaba na  maabara ya kompyuta ambalo litakuwa na ghorofa 2. Jengo lingine ni jengo la kijamii, ambalo litakuwa mahusisi kwa kutoa huduma za kijamii kama sehemu za kutoa Fedha (ATM), migahawa ya vyakula, sehemu za kufanya mazoezi na sehemu za maduka. Ameongeza kuwa eneo lingine litakalojengwa ni eneo la viwanja vya michezo, maegesho ya magari, sehemu za kupumzika ( vimbweta) na mitaro ya kupitisha maji.


Mkurugenzi huyo wakati akiwasilisha ripoti hiyo amesema maelezo hayo ni maandalizi ya tangu awali kama ilivyokuwa imaandaliwa,hivyo kuna uwezekano kukawa na mabadiliko ya ujenzi kutoka na madiliko ya thamani ya pesa au maoni ya wahundisi watakao husika katika ujenzi.

Mpango wa miradi ya kuendeleza vyuo vikuu nchini ( HEET PROJECTS) utakuwa wa miaka mitano na utasaidia vyuo vya elimu ya juu 14.

Matangazo

  • RIPOTI YA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI February 13, 2024
  • Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 February 19, 2024
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji daftari la kudumu la mpiga kura. August 31, 2024
  • Tangazo la Shughuli ya Muda Mfupi kwaajili ya Uchaguzi September 17, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RC Kihongosi Akabidhi Pikipiki na Vifaa vya Kidijitali Kuboresha Huduma za VVU Bariadi.

    May 08, 2025
  • BARIADI DC KUANZA KUTOA DOZI YA PILI YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO (IPV2) KUANZIA MEI 2025

    April 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO KWAAJILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI AONGOZA KIKAO CHA KUJIRIDHISHA JUU YA MAOMBI YA KUGAWA JIMBO LA BARIADI

    April 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Bariadi, akifafanua kwa undani Banuai ya Halmashauri Wilaya ya Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Matangazo
  • Habari
  • TANGAZO LA KAZI HALMASHAURI YAWILAYA BARIADI

Kurasa Husishi

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • Wizara ya Fedha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Bariadi

    Anuani: 109-Bariadi

    Simu: 028 2700012

    Simu: +255683705815

    Barua Pepe: info@bariadidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2019 Bariadi District Council . All rights reserved.